Refa wa kandanda apigwa risasi na kuuawa Mogadishu, Somalia
Mwamuzi maarufu katika mchezo wa kandanda nchini Somalia amepigwa risasi na kuuawa karibu na nyumbani kwake mjini Mogadishu.
Osman Jama Dirah, ambaye alisimamia mechi za kanda na kimataifa, aliuawa akiondoka msikitini kurejea kwake nyumbani katika mtaa wa Wardhigley.
Taarifa zinasema wanaume wawili waliokuwa na bastola walimfatulia risasi mara kadha.
Mchezaji wa zamani wa timu ya taifa ya Somalia Anas Ali Mohamud amenukuliwa akisema aliwaona washambuliaji wakiondoka eneo la mauaji.
Anasema maafisa wa usalama walifika eneo hilo baadaye lakini kufikia sasa hawajafanikiwa kuwakamata wahusika.
Labels: By Xoxher Hero
0 Comments:
Post a Comment
Subscribe to Post Comments [Atom]
<< Home