Angalia hapa tarehe ambayo jua litapatwa tena Tanzania
Jumatatu 21 Agosti 2017 mamilioni ya Wamarekani watashuhudia moja ya tukio kubwa zaidi ya jua kupatwa na mwezi katika kipindi cha karibu miaka 100.
Takwimu zimetoka kwa Shirika la Anga za Juu la Marekani.
Kupatwa kwa jua kikamilifu 21 Agosti
Jua litapatwa kikamilifu leo kuanzia maeneo ya kaskazini mashariki mwa Bahari ya Pasifiki kabla ya kuanza kuonekana ardhini katika Lincoln Beach, Oregon mwendo wa saa 10:16 saa za huko (18:16 BST/Saa mbili jioni Afrika Mashariki).
Ukanda ambapo kutakuwa na giza totoro utapitia Amerika Kaskazini kwa dakika 90 hivi na kupitia maeneo ya Oregon, Idaho, Wyoming, Nebraska, Missouri, Illinois, Kentucky, Tennessee, North Carolina, South Carolina na Georgia.
Majimbo mengine nchini Canada na mataifa mengine ya Amerika Kusini na Kati pia yatashuhudia kupatwa kwa jua kisehemu.
Aidha, baadhi ya nchi za Afrika Magharibi na Ulaya magharibi pia zitashuhudia kupatwa kwa jua kisehemu. Lakini nchini Uingereza, katika maeneo mengi, jua litazibwa asilimia 4 pekee mwendo wa saa 20:00 BST.
Hili hapa ni jedwali la kuonesha ni lini mataifa mbalimbali Afrika yatashuhudia jua likipatwa hivi akribuni.
Labels: BBC news, By Xoxher Hero
0 Comments:
Post a Comment
Subscribe to Post Comments [Atom]
<< Home